Saturday, September 1, 2012

John Legend - Tonight (Best You Ever Had) feat. Ludacris




Best Song 2012, I can listean to da song the all day I Luv it

UCHAGUZI DRFA OKTOBA 14


KAMATI ya uchaguzi ya chama cha soka mkoa Dar es Salaam, DRFA leo kimetangaza utaratibu wa uchaguzi wa chama hicho unaotarajiwa kufanyika Oktoba 14 mwaka huu, baada ya kusimamishwa shirikisho la mpira wa miguu nchini TFF, kutokana na kasoro zilizokuwemo katika katiba yao.

Kamati imeamua kutangaza mapema fursa za wanaotaka kuwania uongozi ndani ya DRFA mapema kabla ya tarehe 3 tuliyopanga awali, ili kutoa wigo mpana zaidi ya wagombea. Septemba 10 itakuwa ni siku ambayo kamati ya uchaguzi itakaa na kuzipitia fomu zote na kuweka wazi kwenye mbao za matangazo majina ya waombaji uongozi DRFA.

Septemba 16 kutoa fursa ya pingamizi kwa waombaji uongozi. Mwisho wa kupokea pingamizi ni Septemba 20 saa 10 alasiri. Pingamizi ziwasilishwe kwa katibu wa kamati ya uchaguzi.

Hakutakuwa na ada katika kuweka pingamizi, bali pingamizi zizingatie matakwa ya ibara ya 11(2) ya kanuni za uchaguzi.

Ratiba hii inaonesha Septemba 26 ni fursa ya kukata rufaa iwapo maamuzi yaliyotolewa na kamati DRFA hayakurishishwa na mrufaa na hiyo itakwenda kwa kamati ya TFF.

Kampeni kwa wagombea zitaanza rasmi Oktoba 4, hadi13 ambapo Oktoba 14 itakuwa uchaguzi.  Pia katika kikao cha kamati ya uchaguzi ya DRFA kilichoketi Septemba 1, imetoa ufafanuzi  kuhusu waliochukua fomu awali kuwa watachukua tena, lakini hawatalipa ada ya kuchukua fomu.

Ada kwa nafasi ya Mwenyekiti, Makamu na Katibu ni Sh. 200,000 wakati nafasi nyingine zote ni Sh.100,000 na kuwa kipengele pekee kilichotakiwa marekebisho cha kiwango cha elimu kimerekebishwa na hakuna sehemu inayosema inayofanana na, bali elimu ya kidato cha nne.

 

 

 

Friday, August 31, 2012

MUSTAFA HASSANALI INVITED TO COLOUR IN THE DESER FASHION WEEK

“Pink Desert Collection” Hassanali’s Fourth collection so far in 2012
Mustafa Hassanali to advocate breast cancer awareness through his work.
Pan African Designer from Tanzania, Mustafa Hassanali has been invited at the 2nd Edition of The Colour in the Desert Fashion Week 2012 in Gaborone for the second year in a row from 31 August to 1 September
“As the only designer from Tanzania to be invited at this prestigious Fashion Week in
Botswana, I am very excited and honored to launch my new collection, the fourth one.
This year 2012, I look forward to use this opportunity to promote our culture and
Strengthen ties existing between Botswana and Tanzania and within Africa at large.”
Stated Mustafa Hassanali
This Collection is named Pink Desert Collection which consists of Mustafa Hassanali |signature Gown but also some pieces of ready to wear and men’s wear that summates the vast richness of this collection by addition of vintage buttons and zips.
The collection is being launched at an opportune moment just as we nearing the month of October which is globally known for breast cancer Awareness.
“I shall use this collection also to advocate Breast Cancer Awareness and the need for every woman to self examine themselves. To think and wear Pink is to be aware of Breast Cancer, a reality which has been the cause of leading cause of death in women.” Concluded Hassanali
 Mustafa Hassanali has already launched 3 Collection in 2012.Afrikalos collection in Lagos Nigeria, Wedding collection in Dar es Salaam, Ramadhan Collection in Dakar, Senegal and has shown at Fashion extravaganza in Kampala, Uganda and Bangalore fashion week in India.

TALENT MISS ILALA YACHENGUA

WAREMBO watano jana usiku, waliwafunika wenzao katika shindano dogo la kategoria ya kipaji Miss Ilala 2012 na kutangazwa kuingia tano bora ambapo mmojawapo atatangazwa mshindi katika fainali ya mashindano hayo,  Septemba 7 mwaka huu.

Katika shindano hilo lilofanyika katika ukumbi wa Nyumbani Lounge, kiukweli warembo hao walionesha uwezo mkubwa kwamba walijiandaa vilivyo katika kuhakikisha kila mmoja anampuki mwenzie, lakini mwishowe watano walitangazwa na majaji Khadija Mwanammbo na Matukio Chuma kuwa wamevuka hatua ya fainali.

Katika kinyanganyiro hicho mrembo Mary Chizi alikuwa kivutio zaidi kwa jinsi alivyoonesha umahiri wake wa wepesi wa kujvingirisha mwili huku Mectilda Martin akizoa ukumbi mzima kwa kurap na huku akiwa ameandana kwa kucheza hata mavazi yanayotumiwa na wasanii wa miondoko hiyo.

Magdalena Munisi haukuwa nyuma kabisa katika kumwigiza mwanamuziki nguli wa marekani, Ciara kwa umahiri wake wa kulitumia jukwaa, lakini kubwa kuliko pia kwa mrembo Amina Sangawe alibuni nguo kwa kutumia vipande viwili vya khanga ambapo aliliunganisha jukwaani kupitia pini nakumvika mmrembo mwenzie. Stella Moris kwa upande wake alionesha ukali kwa kuimba.

Mshindi wa taji hilo, atatajwa katika kilele cha shindano la Miss Ilala 2012 kwenye ukumbi huo huo, Septemba 7, mwaka huu. Shindano hilo lililoanza saa 3;00 usiku, lilipambwa na burudani ya bendi ya mapacha watatu na mastaa kibao wa bongo walikuwepo.

Warembo hao, wamekuwa wakijifua kwa takriban wiki nne sasa chini ya wakufunzi, Slyvia Mashuda ambaye ni Miss Tanzania namba mbili mwaka 2008 na Miss Ilala wa mwaka huo, na Neema Mbuya na Dickson Daudi wa THT katika shoo.

Miss Ilala, yenye rekodi ya kutoa warembo wanne waliotwaa taji la Miss Tanzania kuanzia mwaka 1999, (Hoyce Temu), 2000 (Jacquline Ntuyabaliwe aka K-Lyne), 2002 (Angela Damas Mutalimwa) na Salha Israel anayeshikilia taji hilo kwa sasa, imepania kuendeleza rekodi yake nzuri mwaka huu.
Miss Ilala inahusisha warembo kutoka vitongoji vya Dar City Center, Tabata na Ukonga na inadhaminiwa na City Sports Lounge, Redd's Premmium Cold, Uhuru One, Dodoma Wine, Nyumbani Lounge, gazeti la Jambo Leo,  100.5 Times FM, Redio ya watu 88.4 Cloud's FM.
 Mrembo Magdalena Munis akicheza kumwigiza mwanamuziki wa Kimarekani Ciara katika shindano hilo.
 Mrembo Mectilda Martin akionesha umahiri wake wa kurap jukwaani.
 Amina Sangawe (kulia) mara baada ya kumaliza gauni lake la ubunifu alilomvika mrembo mwenzie Elizaberth Perty alilotumia khanga kushikizia na pini
 Kama hawapo Nyumbani Lounge wakurugenzi wa City Sports Lounge, Juma Pinto(kushoto) na Benny Kisaka wakati wa shoo hiyo

POLKA DOTS

kardashian Collection


 Am so inlove with this dress, its classy n sexy
 

KILEMBA TREND

Nancy Sumari Looking Good sanaa, this style ts so inn at the moment u can actually wear da kilemba in different occasions and still look good!!!!!




MARTIN KADINDA NDANI YA AFRICA NEW YORK FASHION WEEK

 Martin kadinda, Mtanzania wakwanza kuonyesha mavazi yake during the new york fashion week, ambayo watu wengi kutoka sehemu tofauti tofauti around the world watakuepo, fashion bloggers pia jadore nawengine wengi!
Diamond dressed by Martin

 Some of Martin Designs
Single Button


Wema ndani ya Single Button by Martin


 

Thursday, August 30, 2012

KAPTENI GADNA G HABASH AANZISHA MASKANI TIMES FM

MTANGAZAJI Super Star bongo, Gadna G. Habash leo ametambulishwa rasmi kuhamia kituo cha redio cha 100.5 Times FM, baada ya kuwa nje ya kazi kwa takriban miaka miwili,  ambako alijikita zaidi katika kuanzisha na kuimarisha mgahawa wa Nyumbani Lounge.
Sauti yenye ubunifu wa hali ya juu katika uendeshaji kipindi cha mume wa mwanamuziki nyota Tanzania, Lady Jaydee 'aka' bint machozi sasa itakuwa ikisikika alichokibuni cha Maskani, kuanzia saa 10:00 jioni hadi saa1:00 usiku, muda ambao utakuwa sawia kabsia na kipindi alichokiasisi akiwa Cloud's FM cha Jahazi.
Kapteni G alikuwa akitangaza kipindi cha Jahazi Clouds kabla ya kubwaga manyanga Novemba mwaka 2010 katika kipindi ambacho redio hiyo ilipoteza mastaa wengi, wakiwemo Fina Mango, George Njogopa na Masoud Kipanya.  
Fina kwa sasa yupo Magic FM na Kipanya alimtangulia Gadna Times FM. Katika mkutano huo wa chakula cha mchana na wanahabari wa vyombo mbalimbali, mbali ya Gadna, Times pia iliwatambulisha wasanii Suzan Ngatwika 'Natasha na mwanae Monalisa kuwa wanaendesha kipindi kiitwacho Mama na Mwana.
 Gadna akizungumza na Waandishi wa Habari katika mgahawa wa City Sports Lounge mchana huu, katikati ya Jiji leo. Wengine kulia kwake ni Scholastica Mazula, Cliffor Ndimbo na Hadija Shaibu 'Dida'. Kulia ni Jabir Saleh.
Gadna kushoto akiwa na Schola na mtangazaji mwingine mpya wa Times, Natasha ambaye anatangaza kipindi cha Mama na Mwana.

DSTV CHANNELS CHANGES



A MOVIE FOR EVERY MOOD!

A NEW ERA FOR MOVIES AS M-NET EXPANDS MOVIE OFFERING ON DStv

August 2012

DStv audiences across Africa are set to get more movie magic as entertainment powerhouse M-Net embarks on an exciting new chapter! From Monday 1 October 2012, the M-Net movie offering on DStv will be expanding to include eight genre-themed movie channels.

The 8 movie channels are themed according to movie type and will include M-Net Movies Premiere,

M-Net Movies Comedy, M-Net Movies Family, M-Net Movies Action Plus, M-Net Movies Drama & Romance and M-Net Movies Showcase. Rounding off the M-Net movie line-up are M-Net Movies Action (previously M-Net Action) and M-Net Movies Stars (previously M-Net Stars).

With the tagline A Movie for Every Mood, audiences can now be assured of a wider choice of the best possible selection of available movies anytime of the day.

This marks a significant evolution in M-Net’s movie line-up that currently encompasses only 2 generic movie channels. The new range of movie channels, which debuts in October, is specifically designed to ensure easy navigation for audiences so they know just where to find their favourite type of movie.

To find out more on each channel, please read on…

· M-Net Movies Premiere (DStv Channel 103): This where you can find the freshest movies appearing on television for the first time. 5 new movies will be screened every weekend on M-Net Movies Premiere and kicking off every weekend on a Friday is 4 of the 5 blockbusters.

· If you like your comedies with a little romance, drama or with slapstick humour, M-Net Movies Comedy (DStv Channel 104) will have you laughing out loud.

· M-Net Movies Family (DStv Channel 105) is the destination for wholesome entertainment for all ages, featuring animation, musicals, fantasy and feel-good family movies will keep both kids and the young at heart engrossed all day.

· Viewers can expect a host of blockbuster movies from Action to Westerns, Horror and Sci-Fi on M-Net Movies Action Plus (DStv Channel 106).

· There is also M-Net Movies Drama & Romance (DStv Channel 107) for those who prefer biographies, thrillers, documentaries and war movies.

· M-Net Movies Showcase (DStv Channel 108) shines the spotlight on specific movies and directors with exciting festivals, themes and box sets. In addition, viewers get to take control and recommend movies with a special viewer’s choice.

(MM1 and MM2 will be replaced with the 6 themed movie channels above)

· All things action will be available on M-Net Movies Action (DStv Channel 110, previously M-Net Action).

· And M-Net Movies Stars (DStv Channel 111, previously M-Net Stars) is the channel for young and old alike. It features modern greats and movie favourites from past and present across a variety of genres from comedy to drama and romance.

PLUS: From the month of October, viewers can look forward to festivals, themed evenings and a viewer’s choice on selected nights across all the channels.

For more information on these exciting new channels, log on to www.dstv.com!

DStv subscribers can also get information on the upcoming DStv channel re-numbering initiative on the DStv website. With DStv launching several new channels in the recent past, the channel re-numbering initiative is focused on ensuring that all channels are grouped as relevant by genres. This will mean that viewers can find the channels that they are looking for easily and quickly. This update of the channel numbers will also allow for future channel growth on DStv.

And to help viewers navigate the channel number changes, DStv is also launching a dedicated channel (DStv channel 198), hosted by Big Brother star IK Osakioduwa. Alternatively simply press OK on your DStv remote and click on the Renumbering section for info.

So sit back, relax and get ready for a world of great movie entertainment…courtesy of M-Net and only on DStv!

Ends.

 


KWA MARA YA KWANZA KABISA NDANI YA MAREKANI..DIAMOND LIVE IN WASHINGTON DC JUMAMOSI HII TAREHE 1 SEPT!

“Kwa mara ya kwanza nitasafiri nje ya nchi na madensa wangu wanne na msemaji mmoja. Sasa hivi hawataki kutembea na kupanda magari wasije wakakosa hiyo safari,” alisema Diamond na kuongeza kuwa baada ya kuumwa, mawazo aliyaweka kwenye mchongo huo hivyo mambo mengine yataendelea ikiwa ni pamoja na kufanya kolabo na mwanamuziki wa kimataifa wa Nigeria, J. Martins

Wednesday, August 29, 2012

HEKALU JIPYA LA MCHUNGAJI DK. GETRUDE RWAKATARE KUFUNGULIWA RASMI

 
 Mama Getrude Rwakatre siku ya Jumapili alikuwa anahamia rasmi katika nyumba yake mpya iliyoko Mbezi Beach jijini Dar es Salaam pembezoni mwa bahari ya Hindi. Waumini wa kanisa hilo wapatao takribani 300 walifika mahali hapo kwa kushuhudia nyumba ya kifahali.

Muonekano wa mbele 
 Mc Harris Kapiga akiwa kazini.
 Mchungaji Getrude Rwakatare akwakaribisha wageni nyumbani kwake.
 MC na mchungaji Haris Kapiga wa Clouds FM

 
 
 
 Kitanda chake cha kulala
 wakati wa misosi kwa wageni

Miduara ikichezwa

 

SERENGETI BOYS SASA KUIVAA MISRI

Timu ya Taifa ya Tanzania chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) sasa itaivaa Misri kwenye raundi ya pili ya michuano ya kuwania tiketi ya kucheza Fainali za 10 za Afrika kwa vijana chini ya miaka 17 zitakazofanyika mwakani nchini Morocco.

Awali Serengeti Boys ilikuwa icheze raundi ya kwanza dhidi ya Kenya, mechi ya kwanza ikichezwa Septemba 9 mwaka huu jijini Dar es Salaam. Hata hivyo, Shirikisho la Mpira wa Miguu la Kenya (FKF) jana lilituma taarifa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) likielezea kujitoa kwenye michuano hiyo.

Serengeti Boys itaanzia nyumbani Oktoba 14 mwaka huu, wakati ya marudiano itachezwa nchini Misri kati ya Oktoba 26-28 mwaka huu. Mshindi baada ya mechi hizo mbili ataingia raundi ya tatu ambayo ndiyo ya mwisho kabla ya kwenda Morocco.

Katika raundi ya tatu ambayo mechi zake zitachezwa katikati ya Novemba na ya marudiano mwisho mwa mwezi huo, mshindi kati ya Tanzania/Misri atacheza na mshindi wa mechi ya Congo Brazzaville dhidi ya Msumbiji/Zimbabwe ambazo zinapambana katika raundi ya kwanza.

Wachezaji wanaounda kikosi cha Serengeti Boys chini ya Kocha Jakob Michelsen ni makipa Abdallah Bakar (Mjini Magharibi), Hamad Juma (Azam) na Peter Manyika (JKT Ruvu).

Mabeki ni Abdallah Salum (Mjini Magharibi), Basil Seif (Morogoro), Hassan Mganga (Morogoro), Ismail Gambo (Azam), Mgaya Abdul (Azam), Miraji Selemani (Polisi Morogoro), Miza Abdallah (Kinondoni), Mohamed Hussein (Azam), Pascal Matagi (Dodoma) na Paul James (Kinondoni).

Viungo ni Farid Musa (Kilimanjaro), Hussein Twaha (Coastal Union), James Mganda (Kipingu Academy), Mbwana Ilyasa (Simba), Mohamed Haroub (Zanzibar), Mohamed Kapeta (Kinondoni), Mudathiri Yahya (Azam), Mzamiru Said (Morogoro) na Selemani Bofu (JKT Ruvu).

Washambuliaji ni Abdallah Kisimba (Mwanza), Calvin Manyika (Rukwa), Dickson Ambunda (Mwanza), Joseph Lubasha (Azam), Kelvin Friday (Azam) na Salvatory Nkulula (Kipindu Academy).

MCHEZAJI AOMBEWA ITC UJERUMANI
Chama cha Mpira wa Miguu cha Ujerumani (DFB) kimetuma maombi ya kupatiwa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) kwa ajili ya mchezaji Robert Makanja ili aweze kucheza mpira wa miguu nchini humo.

DFB imetuma maombi hayo Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ili kumwezesha mchezaji huyo kuichezea timu ya TUS Ahausen, Hessischer FuBall-Verband ambayo hata hivyo haikuelezwa iko ligi ya daraja gani nchini humo.

Kwa mujibu wa Mkuu wa Mashindano wa DFB, Markus Stenger, Mtanzania huyo ameombewa hati hiyo kama mchezaji wa ridhaa kwa maelezo kuwa hakuwahi kusajiliwa na klabu yoyote nchini.

TFF inafanyia kazi maombi hayo na hati hiyo itatolewa mara baada ya taratibu husika kukamilika ikiwemo kubaini kama kweli mchezaji huyo hakuwahi kusajili na klabu yoyote hapa nchini.

TALENT MISS ILALA, ALHAMIS HII NYUMBANI LOUNGE

VIMWANA 14 wanaotarajiwa kupanda jukwaani kuwania umalkia wa Kanda ya Manispaa ya Ilala, Redds Miss Ilala 2012 kesho Agosti kwenye ukumbi wa Nyumbani Lounge, watamenyana kuwania taji la mrembo mwenye kipaji, ikiwa ni sehemu ya kuelekea shindano lenyewe litakalofanyika Septemba 7, mwaka huu.

Warembo hao ambao wamejiandaa vilivyo kila mmoja akiwa amejiandaa katika kipengele anachokimudu zaidi, wamekuwa wakipata maelekezo ya kuboresha wanachotaka kukifanya kwa walimu wa fani ya sanaa mbalimbali.

Katika shindano hilo litakaloanza saa 2;00 usiku, bendi ya mapacha watatu watatumbuiza ndani ya ukumbi huo kwa kiingilio cha sh 10,000 tu. Redds Miss Ilala inayoshikilia taji la Miss Tanzania kupitia mrembo wake, Salha Israel, tumejiandaa vilivyo mwaka huu kuonesha mambo mengi yatakayowavutia mashabiki siku ya shindano hilo.

Mbali ya maandalizi ya shoo, pia mwaka huu tumejiandaa vizuri kuhakikisha taji hilo linaendelea kubaki katika manispaa yetu na ili katika kujiweka sawa na hilo, warembo wamekuwa wakijifua kwa takriban wiki nne sasa chini ya ukufunzi wa Slyvia Mashuda tayari kwa shindano hilo litakalofanyika Septemba 7 kwenye ukumbi wa nje wa Nyumbani Lounge.

Slyvia ni Miss Tanzania namba mbili mwaka 2008, akiwa Miss Ilala wa mwaka huo akishiriana na Neema Mbuya sanjari na Dickson Daudi wa THT katika shoo. Miss Ilala ambayo tumeshatoa warembo wanne waliotwaa taji la Miss Tanzania kuanzia mwaka 1999, (Hoyce Temu), 2000 (Jacquline Ntuyabaliwe aka K-Lyne), 20029( Angela Damas Mutalimwa) na  Vodacom Miss Tanzania, Salha Israel anayeshikilia taji hilo.

Warembo hao kutoka vitongoji vya Dar City Center, Tabata na Ukonga wamekuwa wakiendelea na mazoezi katika Club ya Nyumbani Lounge, iliyopo maeneo ya Namanga, Dar es Salaam. Washiriki hao ni pamoja na  Mary Chizi, Matilda Martin, Magdalena Munisi, Suzan Deodatus, Whitness Michael, Stella Moris na Elizaberth Pertty.

Warembo wengine ni Wilmina  Mvungi, Zawadi Mwambe, Rehema Said, Diana Simon, Amina Sangwe, Noela Michael na Phillios Lemi.

Mbali ya Uhuru One, Wadhamini wengine katika mashindano hayo ni pamoja na Dodoma Wine, City Sports Lounge, gazeti la Jambo Leo, Nyumbani Lounge, 100.5 Times FM, Redio ya watu 88.4 Cloud's FM na Redds Premmium Cold.

Tuesday, August 28, 2012

NJE YA TANZANIA KUSHUDIA MISS ILALA

MASHABIKI wa urembo nchini na wale waliopo ughaibuni, kwa mara ya kwanza watalishuhudia moja shindanao la kumsaka mrembo wa Ilala 'stream live', kazi itakayofanywa kitaalam zaidi na kampuni ya Uhuru One.

Mbali ya mashabiki kupata faida hiyo ya kuoneshwa moja kwa moja kupitia mtandao, lakini faida kubwa kamati ya Miss Ilala imezingatia mchango wa wadhamini matangazo yao kuonekana nje ya mipaka ya jiji la Dar es Salaam na ughaibuni.

Ilala, ambao tunashikilia taji la Miss Tanzania kupitia Salha Israel, mwaka huu tumejiandaa vilivyo kuhakikisha taji hilo linaendelea kubaki katika manispaa yetu na ili katika kujiweka sawa na hilo, warembo wamekuwa wakijifua kwa takriban wiki nne sasa chini ya ukufunzi wa Slyvia Mashuda tayari kwa shindano hilo litakalofanyika Septemba 7 kwenye ukumbi wa nje wa Nyumbani Lounge.

Slyvia ni Miss Tanzania namba mbili mwaka 2008, akiwa Miss Ilala wa mwaka huo akishiriana na Neema Mbuya sanjari na Dickson Daudi wa THT katika shoo. Miss Ilala ambayo tumeshatoa warembo wanne waliotwaa taji la Miss Tanzania kuanzia mwaka 1999, (Hoyce Temu), 2000 (Jacquline Ntuyabaliwe aka K-Lyne), 20029( Angela Damas Mutalimwa) na  Vodacom Miss Tanzania, Salha Israel anayeshikilia taji hilo.

Warembo hao kutoka vitongoji vya Dar City Center, Tabata na Ukonga wamekuwa wakiendelea na mazoezi katika Club ya Nyumbani Lounge, iliyopo maeneo ya Namanga, Dar es Salaam. Washiriki hao ni pamoja na  Mary Chizi, Matilda Martin, Magdalena Munisi, Suzan Deodatus, Whitness Michael, Stella Moris na Elizaberth Pertty.

Warembo wengine ni Wilmina  Mvungi, Zawadi Mwambe, Rehema Said, Diana Simon, Amina Sangwe, Noela Michael na Phillios Lemi.

Mbali ya Uhuru One, Wadhamini wengine katika mashindano hayo ni pamoja na Dodoma Wine, City Sports Lounge, gazeti la Jambo Leo, Nyumbani Lounge, 100.5 Times FM, Redio ya watu 88.4 Cloud's FM na Redds Premmium Cold.


SERENGETI BOYS, KENYA KUCHEZA AZAM COMPLEX

Mechi ya kwanza ya raundi ya kwanza kuwania tiketi ya kucheza Fainali za 10 za Afrika kwa vijana chini ya miaka 17 zitakazofanyika mwakani nchini Morocco kati ya Tanzania (Serengeti Boys) na Kenya itachezwa Septemba 9 mwaka huu Uwanja wa Azam Complex ulioko Chamazi, Dar es Salaam.

Tayari Serengeti Boys chini ya Kocha Jakob Michelsen na Msaidizi wake Jamhuri Kihwelo ikiwa na wachezaji 28 iko kambini jijini Dar es Salaam tangu jana (Agosti 27 mwaka huu) kujiandaa kwa mechi hiyo itakayoanza saa 10 kamili jioni.

Wachezaji waliko kambini ni makipa Abdallah Bakar (Mjini Magharibi), Hamad Juma (Azam) na Peter Manyika (JKT Ruvu). Mabeki ni Abdallah Salum (Mjini Magharibi), Basil Seif (Morogoro), Hassan Mganga (Morogoro), Ismail Gambo (Azam), Mgaya Abdul (Azam), Miraji Selemani (Polisi Morogoro), Miza Abdallah (Kinondoni), Mohamed Hussein (Azam), Pascal Matagi (Dodoma) na Paul James (Kinondoni).

Viungo ni Farid Musa (Kilimanjaro), Hussein Twaha (Coastal Union), James Mganda (Kipingu Academy), Mbwana Ilyasa (Simba), Mohamed Haroub (Zanzibar), Mohamed Kapeta (Kinondoni), Mudathiri Yahya (Azam), Mzamiru Said (Morogoro) na Selemani Bofu (JKT Ruvu).

Washambuliaji ni Abdallah Kisimba (Mwanza), Calvin Manyika (Rukwa), Dickson Ambunda (Mwanza), Joseph Lubasha (Azam), Kelvin Friday (Azam) na Salvatory Nkulula (Kipindu Academy).

Mechi ya marudiano itachezwa jijini Nairobi, Kenya kati ya Septemba 21, 22 na 23 mwaka huu. Timu itakayofanikiwa kusonga mbele itacheza raundi ya pili dhidi ya Misri. Mechi ya kwanza itachezwa nyumbani kati ya Oktoba 12, 13 na 14 mwaka huu wakati ya marudiano itakuwa kati ya Oktoba 26, 27 na 28 mwaka huu.
Misri ni kati ya timu 17 zilizoingia moja kwa moja raundi ya pili. Nyingine ni Afrika Kusini, Algeria, Burkina Faso, Cameroon, Congo Brazzaville, Cote d’Ivoire, Gabon, Gambia, Ghana, Guinea, Mali, Rwanda, Senegal, Sierra Leone, Tunisia na Zambia.

KAMATI YA SHERIA KUPITIA USAJILI SEPT 2
Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji chini ya Mwenyekiti wake Alex Mgongolwa inatarajia kukutana Jumapili (Septemba 2 mwaka huu) kupitia usajili wa wachezaji kwa msimu wa 2012/2013.

Usajili utakaopitiwa ni wa klabu za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na Lidi Daraja la Kwanza (FDL) ambapo Kamati itapitia pingamizi zilizowasilishwa na klabu mbalimbali dhidi ya wachezaji waliosajiliwa na klabu zingine.

PEARL

 


ANIMAL PRINT DRESSES

 
 kim as always looking good in animal print
janifer balaa

SIMPLE BUT STUNNING

 the outfit mavelous
I luv da shoes n da bag simple but gorgeous

MUSTAFA HASSANALI "PINK DESERT COLLECTION" ON 31ST AUG-1ST SEPT 2012


Monday, August 27, 2012

Christian Louboutin

 
I luv da shoes jadore' is killing it
 

salma kikwete, migiro

Mwenyekiti wa taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) Mama Salma Kikwete akiwa na aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Dkt Asha-Rose Migiro baada ya Mama Kikwete kuzindua Mpango wa Kasi ya Uwezeshaji wa Wanawake na Wasichana Agosti 24, 2012 katika ukumbi wa Kilimanjaro Hyatt Regency jijini Dar es salaam.

RAIS KIKWETE NA FAMILIA YAKE WAHESABIWA KATIKA SENSA YA WATU NA MAKAZI


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na mkewe Mama Salma Kikwete na familia yake akijibu maswali toka kwa karani wa sensa ya wazu na makazi Bw. Clement Ngalaba jana Agosti 26, 2012
wakati alipojiunga na mamilioni ya Watanzania katika zoezi hilo lililofanyika kwa mafanikio makubwa nchi nzima.

KOMBAINI COPA COCA-COLA KWENDA 'SAUZI'

Kombaini ya Copa Coca-Cola Tanzania (Dream Team) yenye wachezaji 16 inatarajia kuondoka kesho (Agosti 28 mwaka huu) asubuhi kwenda Afrika Kusini kwenye kambi itakayokuwa chini ya makocha wa Chelsea.

Makocha watano kutoka timu ya Chelsea ya Uingereza ndiyo watakaoongoza kambi maalumu ya kimataifa ya Copa Coca-Cola yenye wachezaji 140 kutoka nchini 15 itakayofanyika jijini Pretoria kuanzia Agosti 28 hadi Septemba 8 mwaka huu.

Robert Luke Udberg, Russel William Banyard, Oliver Staurt Woodall, Shane Jason Hughes na Dean Aaron Steninger kutoka Chelsea FC Foundation ndiyo wanaounda jopo hilo la makocha litakalowanoa vijana hao wenye umri chini ya miaka 17.

Wachezaji wanaounda Dream Team iliyotokana na michuano ya Copa Coca-Cola iliyofanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Juni 24 hadi Julai 15 mwaka huu ni Abrahman Said Mohamed (Zanzibar), Ayubu Alfan (Dodoma), Baker Hamad (Tanga), Edward Joseph (Ruvuma), Hassan Kabunda (Temeke) na Joseph Chidyalo (Dodoma).

Wengine ni Mtalemwa Katunzi (Morogoro), Mwarami Maundu (Lindi),  Nankoveka Mohamed (Ilala), Nelson Peter (Morogoro), Rajab Rashid (Mwanza), Said Ramadhan (Kagera), Shiza Kichuya (Morogoro), Shukuru Msuvi (Temeke), Tanganyika Suleiman (Kigoma) na Tumaini Baraka (Kilimanjaro).
 
Nchi nyingine zitakazokuwa na washiriki katika kambi hiyo ni wenyeji Afrika Kusini, Burundi, Cameroon, Congo Brazzaville, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Kenya, Lesotho, Malawi, Msumbiji, Nigeria, Swaziland, Uganda, Zambia na Zimbabwe.

Hii ni mara ya sita mfululizo kwa kampuni ya Coca-Cola kupeleka Dream Team kwenye kambi za kimataifa. Mwaka 2007 na 2008, timu hiyo ilikwenda Brazil wakati mwaka 2009, 2010 na 2011 ilikuwa Afrika Kusini.

Arsenal wanavyolia na Wenger

Kilio cha mashabiki wa Arsenal

Wasanii wa luninga walipoting​a Fiesta Moshi

 Wasanii wa luninga kutoka kushoto; Aunt Ezekiel, Vicent Kigosi 'Ray', Wema Sepetu, Hartman Mbilinyi na Steve Nyerere walipohudhuria uzinduzi wa Fiesta 2012 jijini Moshi.
Wema Sepetu na Aunt Ezekiel kwenye Fiesta

WANAMITINDO KWA AJILI YA MAONYESHO YA MBUNIFU MAARUFU NCHINI, ALLY RHEMTULLAH.

 Wanamitindo wa kiume wakipita mbele ya majaji wakati wa kusaka wanamitindo wa mbunifu maarufu nchini, Ally Rhemtullah.
Mwanamitindo wa kike akipita mbele ya majaji

Mbunifu Ally Rhemtullah akifuatilia kazi hiyo

Majaji waliofanya Usaili wa kutafuta wanamitindo watakaoshiriki kwenye Onyesho la Mavazi la Ally Rehmtullah Collection 2013 litakalofanyika tarehe 8 September 2012 wakibadilishana mawazo kabla ya kuanza usaili huo.