Friday, August 3, 2012

DRESS TO KILL





Kim K

HIJAB TREND






RAIS KIKWETE ATOA KIFUTA JASHO CHA NG'OMBE KWA WANANCHI WA MONDULI

SERIKALI itakuwa inagawa ng’ombe 1500 kila mwezi kwa wananchi wa wilaya tatu za Mkoa wa Arusha kama kifuta jasho cha kupoteza kiasi cha karibu mifugo 800,000 iliyopotea kutokana na ukame na athari zake mwaka 2008/2009.

Ahadi hiyo imetolewa leo, Alhamisi, Agosti 2, 2012 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete wakati alipozindua Mradi wa Serikali wa Uwezeshaji Mifugo kwa waliopotelewa mifugo yote katika Wilaya ya Monduli kwenye sherehe iliyofanyika Makuyuni wilayani humo.

Katika uzinduzi huo uliohudhuriwa na viongozi wa Mkoa wa Arusha wakiwemo wakuu wa wilaya na wabunge wa mkoa huo, Rais Kikwete amegawa ng’ombe 500 kwa kundi la kwanza la wananchi ikiwa ni mitamba minne na dume moja la kisasa kwa kaya 16 za mwanzo.

Uzinduzi huo ni wa pili kufanywa na Rais Kikwete chini ya Mradi huo wa kwanza wa aina yake kubuniwa na Serikali katika historia na wenye thamani ya sh. Bilioni 12.9.
Februari 19, mwaka huu, Rais Kikwete alizindua Mradi kama huo katika Wilaya ya Loliondo kwenye sherehe zilizofanyika mjini Loliondo. Kesho Agosti 3, 2012 Rais Kikwete anatarajiwa kuendelea na zoezi hilo katika mji wa Loliondo

JK MONDULI


Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Wananchi wa kijiji cha Makuyuni,Wilayani Monduli leo wakati alipofika kuzindua mpango wa kugawa ng'ombe 1500 kila mwezi kwa wananchi wa wilaya tatu za Mkoa wa Arusha kama kifuta jasho cha kupoteza kiasi cha mifugo 800,000 kutokana na ukame na athari zake mwaka 2008/2009.
 
Rais Jakaya Kikwete akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Makuyuni,Wilayani Monduli mchana wa leo wakati alipofika kuzindua mpango wa kugawa ng'ombe 1500 kila mwezi kwa wananchi wa wilaya tatu za Mkoa wa Arusha kama kifuta jasho cha kupoteza kiasi cha mifugo 800,000 kutokana na ukame na athari zake mwaka 2008/2009.

Rais Jakaya Kikwete akimkabidhi ng'ombe mmoja wa wakaazi wa Monduli walioathririka na ukame mwaka 2008/2009 ambapo walipoteza mifugo yao yote. Hafla hii imefanyika leo katika kijiji cha Makuyuni,Wilayani Monduli.

Thursday, August 2, 2012

HERMES FOR LADIES








For the ladies you should definitely own one or more,, zipo classic!

Wednesday, August 1, 2012

OFFICIAL VIDEO-LEKA DUTIGITE VIDEO-KIGOMA ALL STARS



Kigoma All Stars-Leka Dutigite -Abdu kiba, Baba Levo, Banana Zorro, Chege, Diamond plantimuz, kigoma all stars, Leka Dutigite, Linex, Makomando, Mwasiti, Ommy dimpoz, Queen Darling,Rachel, Zitto Kabwe.
In this Video the beuty of kigoma is well seen i love the water fall and everything in this video, bigup to all Kigoma All Stars mmetokelezea!!!!!!!!!!1

TATOO DESIGNS






Choose your favorite

Tuesday, July 31, 2012

VICTORIA BECKHAM'S DESIGNS










QUOTES OF THE DAY


TAJIRIKA NA JAMBO LEO

Kampuni ya Jambo Concepts inayochapisha magazeti ya Jambo Leo, Staa Spoti na jarida la kila mwezi la jambo Brand Tanzania, kwa kushirikiana. a TSN Supermarket wameandaa bahati nasibu (promotion) ambayo itaendeshwa kwa muda wa miezi mitatu ikishirikisha wasomaji walio zaidi ya miaka 18.

Akizungumza na Waandishi wa Habari katika mgahawa wa City Sports Lounge, Mkurugenzi wa Jamboleo Bw. Benny Kisaka amesema msomaji wa gazeti hiloatatakiwa kukata kuponi itakayokuwa inapatikana ukurasa wa pili wa gazeti na kukusanya kuponi za matoleo saba mfululizo.
Mshindi wa kwanza katika bahati Nasibu hiyo atapata Bajaaj yenye thamani ya shilingi milioni 5,500,000/=, mshindi wa Pili atapata Sofa Set yenye thamani ya shilingi milioni 2,000,000/= huku Mshindi wa tatu akijinyakulia TV Flat Screen ya Inchi 32 yenye thamani ya shilingi 850,000/= wakati mshindi wa Nne ataambulia jokofu(fridge) yenye thamani ya shilingi 650,000/.
Gazeti hilo linaloandika habari za siasa, uchumi, jamii, burudani na michezo lilianza kutoka June 4 mwaka 2009, kila siku ambapo mwezi mmoja uliopita walianzisha gazeti jingine la linaloandika habari za michezo na burudani pekee, likiwa linatoka mara moja kwa wiki siku za Jumapili

 Mkurugenzi wa Gazeti la Jamboleo Bw. Ben Kisaka (wa pili kulia) akizungumzia project mpya ya Jambo Concept ambapo amesema katika kufurahia mafanikio ya miaka 3 na nusu ya kushiriki kikamilifu katika Tasnia hii ya habari wameamua kuandaa utaratibu wa kusheherekea na kufurahia pamoja kwa kuwashirikisha na kuwanufaisha wasomaji wa gazeti hilo linalotoka kila siku. Wa kwanza kushoto ni Afisa Masoko wa TSN Roselyn Benny, Meneja Mkuu wa TSN Group Bw. Emmanuel Ngallah na Kulia ni Meneja Mkuu Jambo Concepts Bw. Ramadhani Kibanike.

Meneja Mkuu wa TSN Group Bw. Emmanuel Ngallah (katikati) akifafanua Promosheni ya tajirika na jambo ambayo itaanza tarehe 1 Agosti mwaka huu ambapo amesema droo zao zitakuwa zikichezeshwa mara mbili kila mwezi. Kushoto ni Afisa Masoko wa TSN Roselyn Benny na Kulia ni Mkurugenzi wa Gazeti la Jamboleo Bw. Ben Kisaka.


MECHI YA NGORONGORO HEROES YAINGIZA

Mechi ya kwanza ya raundi ya pili kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika kwa vijana chini ya umri wa miaka 20 kati ya Tanzania (Ngorongoro Heroes) na Nigeria (Flying Eagles) iliyochezwa juzi (Julai 29 mwaka huu) imeingiza sh. 12,901,000.

Fedha hizo zimepatikana kutokana na watazamaji 3,377 waliokata tiketi kushuhudia pambano hilo lililochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Sehemu iliyoingiza watazamaji wengi ilikuwa viti vya bluu na kijani ambapo 2,697 walikata tiketi kwa kiingilio cha sh. 3,000 kila mmoja. Viingilio vingine katika mechi hiyo vilikuwa sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, sh. 10,000 kwa VIP C na B, na sh. 15,000 kwa VIP A iliyoingiza watazamaji 21.

Mgawanyo wa mapato hayo ni kama ifuatavyo; asilimia 18 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ilikuwa sh. 1,967,949.15, gharama ya kuchapa tiketi sh. 2,250,000, gharama za waamuzi na kamishna wa mechi hiyo sh. 760,000 na ulinzi na usafi kwa Uwanja wa Taifa sh. 2,350,000.

Malipo kwa Wachina (Beijing Construction) sh. 2,000,000, asilimia 20 ya gharama za mchezo ni sh. 714,610.17, asilimia 10 ya uwanja sh. 357,305.08, asilimia 5 ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) sh. 178,652.54 na asilimia 65 ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) sh. 2,322,483.05.

Mechi ya marudiano ya michuano hiyo ambayo fainali zake zitafanyika mwakani nchini Algeria itachezwa Agosti 12 mwaka mjini Ilorin, Jimbo la Kwara, Nigeria.

PONGEZI KWA UONGOZI MPYA SIREFA
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linatoa pongezi kwa uongozi mpya wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Singida (DOREFA) uliochaguliwa katika uchaguzi uliofanyika Julai 28 mwaka huu.

Ushindi waliopata viongozi waliochaguliwa kuongoza chama hicho unaonesha jinsi wajumbe wa Mkutano Mkuu wa SIREFA walivyo na imani kubwa kwao katika kusimamia mchezo huo mkoani Singida.

TFF inaahidi kuendeleza ushirikiano wake kwa Kamati ya Utendaji ya SIREFA chini ya uenyekiti wa Baltazar Kimario ambaye amechaguliwa kwa mara ya kwanza.

Uongozi huo mpya una changamoto nyingi, kubwa ikiwa ni kuhakikisha unaendesha shughuli za mpira wa miguu mkoani Singida kwa kuzingatia katiba ya SIREFA pamoja na vyombo vya mpira wa miguu vilivyo juu yake.

Pia tunatoa pongezi kwa Kamati ya Uchaguzi ya SIREFA na Kamati ya Uchaguzi ya TFF kwa kuhakikisha uchaguzi huo unaendeshwa kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi za wanachama wa TFF.

Viongozi waliochaguliwa katika uchaguzi huo uliofanyika Chuo Cha Maendeleo ya Jamii Singida ni Baltazar Kimario (Mwenyekiti), Hussein Mwamba (Katibu Mkuu), Gabriel Gunda (Katibu Msaidizi), Gabriel Mwanga (Mhazini), Hamisi Kitila (Mjumbe wa Mkutano Mkuu TFF), Omari Salum (Mwakilishi wa Klabu TFF), Yagi Kiaratu na Dafi Dafi (wajumbe wa Kamati ya Utendaji).

Nafasi za Makamu Mwenyekiti, Mhazini Msaidizi na wajumbe wawili wa Kamati ya Utendaji zitajazwa katika uchaguzi mdogo utakaofanyika baadaye.

MICHELSEN AITA 22 KAMBI YA COCA-COLA
Kocha wa timu za Taifa za vijana za Tanzania, Jakob Michelsen ameita wachezaji 22 kwa ajili ya michuano ya kimataifa ya Coca-Cola itakayofanyika baadaye mwaka huu nchini Afrika Kusini.

Baadaye watachujwa na kubaki 16 ambao ndiyo watakaokwenda kwenye michuano ya Afrika Kusini. Wachezaji waliochaguliwa wametokana na michuano ya Copa Coca-Cola iliyofanyika jijini Dar es Salaam na mkoani Pwani kuanzia Juni 24- Julai 2 mwaka huu.

Wachezaji walioitwa ni Abdulrahman Mandawanga (Dodoma), Abraham Mohamed (Mjini Magharibi), Ayoub Alfan (Dodoma), Bakari Masoud (Tanga), Daniel Justin (Dodoma), Denis Dionis (Ilala), Edward Songo (Ruvuma), Fikiri Bakari (Tanga), Hassan Kabunda (Temeke), Joseph Chidyalo (Dodoma), Mutalemwa Katunzi (Morogoro) na Mwarami Maundu (Lindi).

Wengine ni Nankoveka Mohamed (Ilala), Nelson Peter (Morogoro), Omari Saleh (Singida), Rajab Rajab (Mwanza), Said Said (Kagera), Shiza Kichuya (Morogoro), Shukuru Msuvi (Temeke), Tanganyika Suleiman (Kigoma), Tumaini Baraka (Kilimanjaro) na William John (Ruvuma).

Pia Michelsen ameongeza wachezaji saba kwenye kikosi cha Serengeti Boys ambacho Septemba mwaka huu kitacheza na Kenya kuwania tiketi ya fainali za vijana wenye umri chini ya miaka 17 za Afrika zitakazofanyika mwakani nchini Morocco.

Wachezaji walioongezwa kwenye kikosi hicho ambao pia wametoka kwenye Copa Coca-Cola ni Abdallah Baker (Mjini Magharibi), Abdallah Kheri (Mjini Magharibi), Calvin Manyika (Rukwa), Dickson Ambunda (Mwanza), Hassan Mganga (Morogoro), Miza Abdallah (Kinondoni) na Mzamiru Said (Morogoro).

WANANCHI WAMEHIMIZWA KUTEMBELEA TOVUTI YA SEKRETARIETI YA AJIRA

Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma, Bw. Xavier Daudi amewataka wahitimu na wale wote wenye kutafuta fursa za ajira Serikalini kujijengea utamaduni wa kutembelea tovuti ya Sekretarieti ya Ajira mara kwa mara kwani kila nafasi za ajira zinapojitokeza huwekwa katika tovuti hiyo ili kutoa fursa kwa wadau walioko nje na ndani ya nchi kuweza kuziona kwa urahisi.

Amesema hayo leo, wakati akiongea na mwandishi wa habari ofisini kwake aliyetaka kujua fursa za ajira zilizoko na taratibu za mchakato wa ajira tangu kutolewa kwa tangazo hadi kupangiwa kituo cha kazi.

Daudi amesema, kwa mfano mwananchi yeyote akitembelea katika tovuti ya Sekretarieti ya Ajira hivi sasa ataona tangazo la kuitwa kazini kwa waombaji kazi waliofaulu katika usaili uliofanyika mwezi Juni, 2012 ambao wanatakiwa kuripoti kwa Waajiri; Wakala wa Vipimo, pamoja na kwa Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii.

Mbali na hilo, pia watakuta tangazo la kuitwa kwenye usaili kwa wale waliokidhi vigezo kulingana na nafasi walizokuwa wameomba kama zilivyokuwa zimetangazwa kwa niaba ya Halmashauri ya Wilaya ya Babati, Chuo cha Mipango Dodoma, Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo, Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo na taasisi nyinginezo.

Aliongeza kuwa katika Tovuti hiyo watakuta pia tangazo la nafasi za kazi 194 zikiwemo nafasi za Wakurugenzi, Wakufunzi Waandamizi wa Vyuo, Wakufunzi Wasaidizi, Wahandisi, Mafundi Sanifu, Wakaguzi wa ndani wa hesabu, Makatibu Mahsusi, Walinzi, Wapishi na kada nyinginezo.

Aidha, amesisitiza ni muhimu kwa waombaji kuzingatia masharti ya tangazo pindi wanapotuma maombi yao kwa njia ya posta ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kupata fursa ya ajira serikalini maana mchakato wa ajira hufuata Sera, Sheria, Kanuni na Taratibu

Katibu wa Sekretarieti ya Ajira alimaliza mahojiano yake kwa kuitaja tovuti ya Sekretarieti ya Ajira kuwa ni www.ajira.go.tz kwa wale wasioifahamu ili waweze kuifahamu.

RAIS KIKWETE AFUTURISHA MKOANI LINDI

Waalikwa wakipakua futari
 Kadhi wa Mkoa wa Lindi ambaye pia ni Shekhe Mkuu wa Mkoa Mohamed Saidi Mushangani akitoa neno la shukurani baada ya futari

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwashukuru waalikwa kwa kuhudhuria katika hafla ya futari aliyoandaa
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na wachungaji waliokuwa miongoni mwa wageni waalikwa
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na wageni wake baada ya futari 

Uganda’s Jannette Evicted in Big Brother Africa 7


BIG BROTHER STARGAME

JANNETTE FALLS SHORT

Lady May, Prezzo, Wati, Talia, Keagan or Kyle could win

The USD 300 000 prize!
Uganda’s Jannette stumbled one step short of the Big Brother StarGame final as she became the 8th housemate to be evicted from the Upville house last night (29 July on DStv Channel 197 & 198 at 20:00 CAT). After managing to dodge nomination for 11 weeks, her luck ran out last Monday as she fell foul of Wati and Lady May – and then received fewer country votes than Kyle, Lady May and Prezzo over the course of this week to see her time in the house come to an end.

Jannette’s departure means that there are six housemates left in the running for the USD 300 000 prize, which will be awarded next Sunday during a spectacular live finale. Lady May, Prezzo, Wati, Talia, Keagan and Kyle need Africa’s votes to determine which of them wins Big Brother StarGame!

Sunday night’s show was as packed with music as it was with drama, as DJ Pita from Uganda’s Sanyu FM spun the decks, Angola’s Young Nucho performed I’m Not Wayne and South African hip-hop stars Jozi rocked the house with Baby Don’t Cry.

It had been a massive week in the Big Brother house as the housemates worked hard to win their ONE Campaign task, and had celebrity shout outs and visitors in the shape of Mary J. Blige, Bono, Nas, Melanie Fiona, Zolani Mahola and Nigeria’s own 2Face Idibia. Kyle had some regrets about putting Keitta up for eviction last week, while Jannette struggled to come to terms with her first nomination.

Last week’s evictees Alex and Keitta have had a busy time since leaving the Big Brother StarGame house and viewers got to hear all about it. Alex said he’d like to be remembered as the guy who was always “chilled out” while Keitta wanted people to think of him as the guy who was the “fun of the house”. Alex learned to respect different people’s opinions and said he had felt particularly close to Yadel. Keitta said his instincts had told him that Kyle had put him up for eviction as part of his ‘save and replace’ decision, which made his eviction “easier”, because in his words: “it’s just a game”.

The time had come, though, for Wati to reveal his ‘save and replace’ decision to his housemates at the end of a pivotal week. IK asked the Malawian to stand and explain his decision. He said that he had realized that there were two Ugandans in the house, so had opted to put Kyle up in his place to test Africa’s feelings about them.

IK didn’t waste time, returning to the house to reveal the result of Africa’s votes this week. After revealing the fates of the rest of the nominees, the spotlight did indeed fall upon the two Ugandans. After a tense wait, IK revealed that the 8th housemate to be evicted from Upville would be Jannette.

“Small Princess” joined IK on stage and discussed her famous dance moves, party antics and alter ego “Lola Fierce”. She admitted that she found Nigerian housemate Ola “really sexy” and said that she had made peace with Wati during the course of her final day as she felt that if she was to be evicted, she wanted to leave the house on good terms. The Ugandan said she had come into Big Brother StarGame to have fun – and certainly did! She was surprised to see that Lady May had nominated her, but had expected a nod from Wati.

It’s all up to the viewers now! You need to vote for the housemate you want to win Big Brother StarGame and take home the USD 300 000 prize! Voting opened immediately after Sunday night’s show and closes at 06:00 CAT on Sunday morning. Each week, viewers stand a chance of winning amazing prize by voting. This week’s winners were: Trishia Simelane (South Africa) who picked up a DStv HD PVR Decoder, Anne Frank (South Africa) won a Big Boy Scooter and Nicci Nthieanduwa (Namibia) who took home a DStv Walka. The following voters also won Nokia mobile phones: Ama Chiraa (Nigeria), Tiosilia Iikela (Namibia), Fiina Nkandi (Namibia), Queen Moshoeu (Botswana) and John Mafabi (Kenya).


There are three ways to vote for the winner of Big Brother StarGame - via web, SMS or WAP. To vote via web or WAP, go to www.africamagic.tv/bigbrother, log in, click ‘Vote’ and then click the appropriate button for the housemate you’d like to see win the big prize. You may vote once per hour.

To vote via SMS, send the word VOTE followed by the housemate's name to the number for your country .SMS’s are charged per specified network tariffs in the various countries. VAS rates apply. Free minutes do not apply. Please note that you can vote 100 times by SMS per telephone number during each voting period.