MABINGWA wa soka Afrika Mashariki na Kati,Yanga wametua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, dakika chache zilizopita bila mlinzi wake mpya aliye gumzo jijini, Mbuyu Twite.
Rwanda wametua wakitokea Rwanda walipokuwa kwa wiki moja kwa ziara ya mechi mbili za kirafiki na kufika Ikulu ya nchi hiyo kwa mwaliko wa Rais Paul Kagame, walicheza mchezo wa mwisho jana kwa kuwafunga Polisi ya nchini humo mabao 2-1, katika mchezo bngali
.
Yanga iliyomsajili Mbuyu Twite kutoka St Eloi Lupopo ya DRC, ingawa alikuwa anachezea APR. Katibu Mkuu wa Yanga, Celestine Mwesigwa amesema kuna mambo anakamilisha na atatua Dar es Salaam ndani ya saa 48 kuanzia leo.
“Tuna imani Jumamosi katika mechi yetu na Coastal Union Uwanja wa Taifa atakuwepo kutambulishwa rasmi,”alisema Mwesigwa. Kuhusu mpango wa Simba SC, kumfungulia kesi Polisi na kumvizia akitua tu nchini imkamate ikidai kuwatapeli dola za Kimarekani 30,000, Mwesigwa alisema; “Simba sio Polisi, na Yanga ni klabu ambayo inafanya mambo yake kwa utaratibu, kwa hivyo hatuna wasiwasi na hilo", alisema Mwesiga.
Mchezaji huyo awali inadaiwa alisaini Simba na kupewa dola za Kimarekani 30,000 lakini baadaye akazirudisha kupitia viongozi wa APR na Lupopo, hatahivyo Simba walikataa kuzipokea.
Kutokana na sintofahamu hiyo, Simba SC waliamua kusajili beki Paschal Ochieng kutoka Kenya, ili kuziba pengo hilo, na hiyo baada ya kuonekana ngome yake ikipwaya katika mashindano ya kombe la Kagame. Katika mchezo wa awali Ijumaa, Yanga waliwachapa mabingwa wa zamani wa Afrika Mashariki na Kati, Rayon Sport mabao 2-0 kwenye Uwanja huo huo wa Amahoro.
Yanga iliyokwenda Rwanda na msafara wa watu 42, wakiwemo wachezaji 28, Maofisa watano wa benchi la Ufundi na viongozi wanane, baada ya kutua wataendelea na mazoezi keshokwenye Uwanja wa sekondari ya Loyola kujiandaa na Ligi Kuu ya Bara, itakayoanza Septemba 15 na Jumamosi itacheza na mabingwa wa Coastal Union ya Tanga kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Monday, August 27, 2012
Manji aongeza dola 20,000 Kagame Cup, kurejea leo mchana
KAMPUNI ya Quality Group Limited, imeongeza dola za Kimarekani 20,000 zaidi ya Sh. Milioni 30 za Tanzania kwenye zawadi za michuano ya soka ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Quality, Yussuf Manji, ambaye pia ni Mwenyekiti wa klabu ya Yanga, alimpa ahadi hiyo rais wa Rwanda, Paul Kagame wakati klabu hiyo ilipomtembelea rais huyo Ikulu ya Rwanda, Alhamisi kijiji cha Urugwiro.
Kwa dola hizo 20,000 sasa kitita cha zawadi za washindi wa michuano hiyo kinatuna hadi kufika dola 80,000 kufuatia dola 60,000 zinazotolewa na rais Kagame. Mwaka 2002, Rais Kagame aliweka rekodi ya kuwa mdhamini wa kwanza kutoa zawadi za mashindani hayo, dola 60,000 ambazo zimekuwa zikigawanywa kwa washindi watatu wa juu.
Mbali na zawadi hizo, rais Kagame pia anatoa dola 15,000 kila mwaka kwa maandalizi ya michuano hiyo na kufanya mchango wake jumla kuwa dola 75,000. Kwa mchango wake huo mkubwa, Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) limeyapa jina la rais huyo mashindano hayo.
Mwakani, michuano ya CECAFA Kagame itafanyika mjini Kigali kuanzia Januari, kwa mujibu wa Katibu wa CECAFA, Nicholas Musonye.Musonye ataenda Kigali mapema mwezi ujao kukutana na viongozi wa Wizara ya Michezo kujadili zaidi kuhusu maandalizi ya michuano hiyo.
Yanga ni mabingwa wa Kombe kwa miaka mfululizo, katika fainali mbili mfululizo zilizofanyika Dar es Salaam hivyo kufanya wawe wametwaa Kombe hilo mara tano jumla na mwakani wataongozana na wapinzani wao wa jadi, Simba SC kwenye michuano hiyo.
Wenyeji Rwanda wanatarajiwa kuwakilishwa na mabingwa mara tatu wa michuano hiyo, APR, ambao mwaka huu waliambulia nafasi ya nne baada ya kufungwa na AS Vita ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) katika mchezo wa kusaka mshindi wa tatu na Polisi.
Wakati huohuo;
Yanga wanatarajiwa kurejea leo Dar es Salaam leo mchana, baada ya kumaliza ziara yao nchini Rwanda jana kwa ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Polisi kwenye Uwanja wa Amahoro jijini Kigali.
Katika mchezo huo, Stefano Mwasika aliisawazishia Yanga, baada ya Fabrice kutangulia kuifungia Polisi na Nahodha Msaidizi, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ akafunga la pili.
Awali Ijumaa, Yanga waliwachapa mabingwa wa zamani wa Afrika Mashariki na Kati, Rayon Sport mabao 2-0 kwenye Uwanja huo huo wa Amahoro.
Siku moja kabla ya mechi hiyo ya kwanza, walitembelea Ikulu ya Rwanda, walipoalikwa na Rais Paul Kagame kupeleka Kombe la Afrika Mashariki na Kati, ambalo tangu mwaka 2002 Rais Kagame amekuwa mfadhili mkuu na mlezi wa mashindano hayo.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Quality, Yussuf Manji, ambaye pia ni Mwenyekiti wa klabu ya Yanga, alimpa ahadi hiyo rais wa Rwanda, Paul Kagame wakati klabu hiyo ilipomtembelea rais huyo Ikulu ya Rwanda, Alhamisi kijiji cha Urugwiro.
Kwa dola hizo 20,000 sasa kitita cha zawadi za washindi wa michuano hiyo kinatuna hadi kufika dola 80,000 kufuatia dola 60,000 zinazotolewa na rais Kagame. Mwaka 2002, Rais Kagame aliweka rekodi ya kuwa mdhamini wa kwanza kutoa zawadi za mashindani hayo, dola 60,000 ambazo zimekuwa zikigawanywa kwa washindi watatu wa juu.
Mbali na zawadi hizo, rais Kagame pia anatoa dola 15,000 kila mwaka kwa maandalizi ya michuano hiyo na kufanya mchango wake jumla kuwa dola 75,000. Kwa mchango wake huo mkubwa, Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) limeyapa jina la rais huyo mashindano hayo.
Mwakani, michuano ya CECAFA Kagame itafanyika mjini Kigali kuanzia Januari, kwa mujibu wa Katibu wa CECAFA, Nicholas Musonye.Musonye ataenda Kigali mapema mwezi ujao kukutana na viongozi wa Wizara ya Michezo kujadili zaidi kuhusu maandalizi ya michuano hiyo.
Yanga ni mabingwa wa Kombe kwa miaka mfululizo, katika fainali mbili mfululizo zilizofanyika Dar es Salaam hivyo kufanya wawe wametwaa Kombe hilo mara tano jumla na mwakani wataongozana na wapinzani wao wa jadi, Simba SC kwenye michuano hiyo.
Wenyeji Rwanda wanatarajiwa kuwakilishwa na mabingwa mara tatu wa michuano hiyo, APR, ambao mwaka huu waliambulia nafasi ya nne baada ya kufungwa na AS Vita ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) katika mchezo wa kusaka mshindi wa tatu na Polisi.
Wakati huohuo;
Yanga wanatarajiwa kurejea leo Dar es Salaam leo mchana, baada ya kumaliza ziara yao nchini Rwanda jana kwa ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Polisi kwenye Uwanja wa Amahoro jijini Kigali.
Katika mchezo huo, Stefano Mwasika aliisawazishia Yanga, baada ya Fabrice kutangulia kuifungia Polisi na Nahodha Msaidizi, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ akafunga la pili.
Awali Ijumaa, Yanga waliwachapa mabingwa wa zamani wa Afrika Mashariki na Kati, Rayon Sport mabao 2-0 kwenye Uwanja huo huo wa Amahoro.
Siku moja kabla ya mechi hiyo ya kwanza, walitembelea Ikulu ya Rwanda, walipoalikwa na Rais Paul Kagame kupeleka Kombe la Afrika Mashariki na Kati, ambalo tangu mwaka 2002 Rais Kagame amekuwa mfadhili mkuu na mlezi wa mashindano hayo.
Friday, August 24, 2012
HAPPY BIRTHDAY TO MY LOVELY SIZ GEE
May your birthday be filled with sunshine and smiles, laughter, love, and cheer, enjoy your day much love tupo pamoja
Ghymkhana wamtimua Ali Mafuruki
Wanachama wa klabu ya Gymkhana juzi walimuondoa Mwenyekiti wa klabu hiyo, Ali Mafuruki na viongozi wenzake na kuundwa kamati ya muda inayokaa madarakani hadi Septemba mwaka huu.
Katika mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa mikutano uliopo ndani ya viwanja Gymkhana Dar es Salaam, walifikia uamuzi wa kumuondoa Mafuruki kwa kuiendesha klabu hiyo kibabe na kuondoa taratibu nyingi ambazo zimekuwa kero kwa wanachama.
Hali iliyomfanya mmoja wa wanachama wa klabu hiyo, ambae ni Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), asiwe mbishi kujiondoa, kwani asiifanye Gymkhana kama Woorlworth ambayo ni moja ya kampuni anazomiliki Mafuruki.
Kufuatia uamuzi huo, wanachama hao wameteua kamati ya muda itakayoongozwa na Victor Kimesera na Makamu wake Erard Mutalemwa, huku manahodha wa michezo yote wanaendelea na nyadhifa zao ambao ndio wanaounda kamati ya utendaji ya Ghymkhana.
Mkutano huo ulianza saa moja na nusu jana usiku huku kukiwa na polisi waliokuwa na lengo la kulinda usalama, lakini ulitawaliwa na jazba ya kumtaka Mafuruki ajiuzuru kwa madai kuiendesha klabu hiyo kinyume na taratibu na maamuzi mengi yamekuwa yake binafsi.
Hata hivyo, Mafuruki baada ya kuingia katika mkutano huo aliwaambia wanachama hao kuwa mkutano huo haukufuata taratibu hivyo maamuzi yoyote ambayo watayachukua yatakuwa yamekiuka katiba ya klabu hiyo na kususia kikao na kuondoka.
Wakati akiondoka wanachama hao walikuwa wakizomea, hali iliyofanya mmoja wa wadhamini wa klabu hiyo Jaji mstaafu, Stella Longway kuchukua jukumu la kuendesha kikao kwa mujibu wa katiba ya klabu hiyo na wanachama kufikia maamuzi ya kuwaondoa viongozi wote wa klabu hiyo.
Klabu hiyo mbali na Jaji Stella inawadhamini wengine wawili ambao ni G. Kilindu na Ritha Akena.Wadhamini hao wana mamlaka ya kufanya kazi hiyo kwa niaba ya wanachama wa klabu hiyo.
Kufuatia uamuzi huo, kamati hiyo ya muda inayoongozwa na Kimesera inatarajia kukutana hivi karibuni pamoja na mambo mengine ni kurudisha ada ya mgeni mwalikwa ‘Guest Fees” kutoka shilingi elfu 10 hadi elfu mbili kama zamani.
Hatua nyingine ni kurudisha utaratibu wa timu za Gymkhana kualika timu za nje kucheza mechi, hali ambayo uongozi wa Mafuruki ulipiga mafuruku kucheza mechi ndani ya viwanja hivyo au timu zinazokuja kulipiwa shilingi elfu 10 kwa kila mchezaji.
Mbali na Mafuruki kama Mwenyekiti, wengingine ni Makamu Mwenyekiti, Profesa Primo Carneiro,Katibu Nicholas Siwingwa, Mweka hazina, Nada Margwe, Mkuu wa wanachama, Santosh Gajjar, Mkuu wa viwanja, David Shambwe, Mkuu wa Bar, Alfred kinshwaga na Joseph Kusaga mkuu wa kitengo cha burudani.
Wengine ni manahodha michezo yao kwenye mabano ni Joseph Tango (Gofu),Inger Njiru (Tenisi),Chukkapalli Sriram (Kriketi),Ivan Tarimo (soka),Deepak Dosh (squashi) na Firoz Yusufunali (snooka)
Lakini wanachama hao wanakusudia kuwarudia wakuu wa vtengo vyote kasoro nafasi ya Mwenyekiti.
Yanga walipotinga Ikulu Rwanda
Rais Paul Kagame wa Rwanda(kulia), akisalimiana na kusikiliza neno la mdhamini wa Yanga, Mama Fatuma Karume wakati rais huyo alipowakiribisha Ikulu, jijini Kigali jana.
Rais Kagame wa Rwanda akisalimiana na kocha wa Yanga, Tom Saintfiet wakati rais huyo alipowakiribisha Ikulu, jijini Kigali jana.
Mwenyekiti wa Yanga, Yusuph Mehmboob Manji(kulia), akimweleza jambo Rais Kagame katika Ikulu ya nchi hiyo jijini Kigali, juzi.
Rais Kagame wa Rwanda(katikati) akishika kombe la Afrika Mashariki na Kati(Kagame Cup) sanjari na kocha wa Yanga, Tom Saintfiet na nahodha Nadir Haroub Carnavaro wakati rais huyo alipowakiribisha Ikulu, jijini Kigali jana.
Mdhamini wa Yanga, Mama Fatuma Karume(katikati) akimkabidhi jezi ya timu hiyo, Rais Kagame Ikulu Kigali, juzi. Kushoto ni Seif Ahmed 'Magari'wakati rais huyo alipowakiribisha Ikulu, jana.
Rais Kagame(kulia), akiteta jambo na Mwenyekiti wa Yanga, Yusuph Manji(Picha zote na Saleh Ally wa Champions.
Rais Kagame wa Rwanda akisalimiana na kocha wa Yanga, Tom Saintfiet wakati rais huyo alipowakiribisha Ikulu, jijini Kigali jana.
Mwenyekiti wa Yanga, Yusuph Mehmboob Manji(kulia), akimweleza jambo Rais Kagame katika Ikulu ya nchi hiyo jijini Kigali, juzi.
Rais Kagame wa Rwanda(katikati) akishika kombe la Afrika Mashariki na Kati(Kagame Cup) sanjari na kocha wa Yanga, Tom Saintfiet na nahodha Nadir Haroub Carnavaro wakati rais huyo alipowakiribisha Ikulu, jijini Kigali jana.
Mdhamini wa Yanga, Mama Fatuma Karume(katikati) akimkabidhi jezi ya timu hiyo, Rais Kagame Ikulu Kigali, juzi. Kushoto ni Seif Ahmed 'Magari'wakati rais huyo alipowakiribisha Ikulu, jana.
Rais Kagame(kulia), akiteta jambo na Mwenyekiti wa Yanga, Yusuph Manji(Picha zote na Saleh Ally wa Champions.
Wednesday, August 22, 2012
NANCY SUMARI WITH HER NEW WEBSITE
visit the website http://mamazuri.com/
Subscribe to:
Posts (Atom)