Wednesday, July 18, 2012

MASANJA MKANDAMIZAJI AWASHA MOTO IRINGA MJINI KATIKA UZINDUZI WA ALBAM YAKE YA HAKUNA JIPYA

Mungu alimtumia Emmanuel Mgaya (Masanja Mkandamizaji au Mchungaji Mtarajiwa) kuwakusanya watu katika Uwanja wa Samora mjini Iringa kushuhudia matendo makuu ya Mungu, ambapo msanii huyu alikuwa akizindua albamu yake ya "Hakuna Jipya" Masanja Mkandamizaji ni mkazi wa jijini Dar es Salaam ni mzawaliwa wa mkoa wa Iringa. Aliamua kufanya tamasha lake katika mkoa aliozaliwa.

Msanja Mkandamizaji aliwakusanya watu kutoka mikoa mbalimbali waliofika  kushuhudia uzinduzi huo. Wasanii wa filamu za kibongo kutoka Dar es Salaam walifika mahali pale kama. Odama, Ray, steve Nyerere, Davina, Chopa Mchopanga, Jacquline Wolper na wengine wengi walifika mahali pale.
Mbali na uimbaji masanja Mkandamizaji ni mchekeshaji katika kituo cha televisheni cha TBC1 "Orijino ze Commedy", kutokana na karama hiyo ya uchekeshaji amepata kibali cha kukubalika katika jamii.

Masanja kwa sasa anajiita "Mchungaji Mtarajiwa" anategemea kuwa mchungaji lakini anasema hajui itakuwa saa ngapi, siku gani na wapi ataanza huduma hiyo, ila anakuomba uzidi kumuombea.

Masanja akisindikizwa na waimbaji mbalimbali kutoka Iringa na mikoa mingine katika uwanja wa samora mjini Iringa

 Masanja Makadamizaji akikagua gwaride lake

 Waimbaji wakiwa pamoja na Masanja Mkandamizaji aliyeshika ubao kama alama ya bunduki

Hapa Mgeni Rasmi akiongea baada ya kuzindua waliokaa ni baadhi ya wabunge wa viti maalum na mkuu wa mkoa wa Iringa.

 JB wa Bongo Movie akiwa ameshika kibaza sauti pamoja na waigizaji wenzake

 JB toka bongo movie akitoa support kwa kununua DVD na Audio Cd

 Diwani wa kata ya kitanzini Manispaa ya Iringa Jesca hakuwa nyuma kutoa support kwa kununua DVD ya album ya HAKUNA JIPYA


Masanja Mkandamizaji na gwaride lake wakiingia jukwaani
 Naibu Waziri wa Elimu Milubo akizindua DVD na VCD

 Vicent Kigosi (Ray) akisalimia wakazi wa Iringa

 Jacquline Waolper akiwa na furaha kuona tamasha linaenda vizuri
Masanja Mkandamizaji akisoma risala

No comments:

Post a Comment