Wednesday, July 4, 2012
Monday, July 2, 2012
PONGEZI KWA RAIS MPYA WA ZFA
Shirikisho la Mpira wa Miguu
Tanzania (TFF) linampongeza Amani Ibrahim Makungu kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa
Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFA) katika uchaguzi uliofanyika juzi (Juni
30 mwaka huu) kwenye hoteli ya Bwawani, mjini Zanzibar.
Ushindi wa asilimia 94
alioupata Makungu ambaye hakuwa na mpinzani katika uchaguzi huo mdogo unaonesha
imani ambayo wajumbe wa Mkutano Mkuu wa ZFA wanayo kwake katika kukiongoza chama
hicho.
Ni matarajio ya TFF kuwa
ushindi huo utatafsiriwa kwa vitendo na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa ZFA na wadau
wa mpira wa miguu Zanzibar kwa kumpa Makungu ushirikiano wa asilimia 100 ili
kuhakikisha Kamati yake ya utendaji inafanya kile kinachotarajiwa na
wengi.
Makungu si mgeni katika mpira
wa miguu, na mchango aliotoa kwa mchezo huo visiwani kabla ya kuwania nafasi
hiyo unatambuliwa na kila anayefuatilia maendeleo ya mpira wa miguu katika
Zanzibar.
TFF tunaahidi kuendelea kutoa
ushirikiano kwa ZFA chini ya Makungu kama ilivyokuwa kwa mtangulizi wake Ali
Ferej Tamim ili kuhakikisha ustawi wa mpira wa miguu visiwani Zanzibar na
Tanzania kwa ujumla.
MISRI YAAHIRISHA MECHI DHIDI
YA NGORONGORO HEROES
Mechi mbili za kirafiki kati
ya timu ya Taifa ya Tanzania kwa vijana wenye umri chini ya miaka 20 (Ngorongoro
Heroes) na Misri zilizokuwa zichezwe mwezi huu zimefutwa.
Chama cha Mpira wa Miguu Misri (EFA) kimetuma
taarifa jana (Julai 1 mwaka huu) kikiomba kusogezwa mbele hadi mwishoni mwa
Agosti baada ya kushindwa kupata usafiri wa ndege kuwahi tarehe ambazo
ilikubaliana na TFF kwa ajili ya mechi hizo.
Ngorongoro Heroes ambayo
tayari iko kambini ilikuwa icheze mechi hizo Julai 3 na 5 mwaka huu jijini Dar
es Salaam ikiwa ni sehemu ya maandalizi kabla ya kuikabili Nigeria katika mechi
ya michuano ya Afrika, Julai 29 mwaka huu.
Mechi nyingine za kirafiki
kwa Ngorongoro Heroes inayofundishwa na Jakob Michelsen zitachezwa Julai 14 na
16 mwaka huu dhidi ya Rwanda.
RUVUMA YAIFANYIA MAUAJI LINDI
7-2
Timu ya Ruvuma imethibitisha
kuwa mwiba mkali katika michuano ya Copa Coca-Cola mwaka huu baada ya leo
asubuhi (Julai 2 mwaka huu) kuishushia Lindi kipigo cha mabao 7-2.
Hadi mapumziko kwenye mechi
hiyo ya kundi A iliyochezwa Uwanja wa Nyumbu mkoani Pwani, washindi ambao kwa
matokeo hayo wamejiweka katika nafasi nzuri ya kucheza 16 bora walikuwa mbele
kwa mabao 3-0.
Waliotikisa nyavu ni Anthony
Christian dakika ya 23 na 50, Edward Songo dakika ya 27, 75 na 86 na Sunday
Leonard dakika ya 32 na 60. Mabao ya Lindi yalifungwa na Salum Mnyamwile dakika
ya 18 kwa njia ya penalti na lingine dakika ya 48 kupitia kwa Mwarami Maundu.
Nayo Tanga imepata ushindi
wake wa kwanza katika michuano hiyo baada ya kuifunga Manyara mabao 2-0 katika
mechi ya kundi B iliyochezwa Uwanja wa Tamco mkoani Pwani. Mabao ya washindi
yalifungwa na Mbwana Musa dakika ya 47 na Issa Mwanga dakika ya 60.
Katika mechi tatu
zilizotangulia Tanga ilitoka sare ya mabao 3-3 na Morogoro, ikapata sare
nyingine ya 1-1 dhidi ya Mwanza, na baadaye 1-1 na Tanga.
Kagera imeendelea kujitutumua
katika michuano hiyo baada ya kupata ushindi wake wa pili katika kundi D kwa
kuilaza Kusini Unguja bao 1-0 katika mchezo uliochezwa Uwanja wa Tanganyika
Packers ulioko Kawe jijini Dar es Salaam.
Bao lake lilifungwa dakika ya
76 na Novati Sebastian. Mechi iliyopita Kagera iliifunga Tabora mabao 2-0 baada
ya kuteleza katika mechi mbili za kwanza kwa kufungwa na Kilimanjaro na
Singida.
Mechi nyingine ilichezwa
Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam ambapo Kinondoni iliibuka na
ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Mara.
UONGOZI TWIGA STARS WATOA
TAMKO
Uongozi wa Twiga Stars
umekana kuwepo vitendo vyovyote vya kinyume na maadili kwa wachezaji wa timu
hiyo ambayo hivi karibuni ilitolewa kwenye mechi za mchujo za michuano ya Afrika
kwa Wanawake (AWC).
Wakizungumza na waandishi wa
habari leo (Julai 2 mwaka huu), Meneja wa Twiga Stars, Furaha Francis na
aliyekuwa Kocha Mkuu wa timu hiyo Charles Boniface Mkwasa wamesema hakuna
vitendo vya aina hiyo.
Mkwasa amesema alikaririwa
vibaya kuhusu suala hilo wakati akiwa kwenye mahojiano na kituo cha televisheni
cha Star Tv kutokana na swali alilokuwa ameulizwa kuhusiana na vitendo
hivyo.
“Ukifuatilia mahojiano yangu
na Star Tv mimi sikusema kuwa kuna vitendo hivyo. Tatizo nadhani lilianzia kwa
magazeti yaliyonukuu kupitia Star Tv, na wala kujiuzulu kwangu hakukuhusiana na
hilo, nimewajibika kama kocha kutokana na kutolewa na Ethiopia,” amesema
Mkwasa.
Naye Furaha Francis amesisitiza kuwa hakuna
vitu vya aina hiyo katika timu hiyo, na kama kuna mtu ana ushahidi na hilo ni
bora akauonesha badala ya kuzungumzia uvumi kuliko ukweli.
“Ukweli ni kwamba si sisi na
wachezaji tu ambao hatukufurahishwa kutolewa na Ethiopia, wapo Watanzania wengi
ambao hawakufurahishwa na matokeo yale. Twiga Stars si timu ya kudumu, haikai na
wachezaji kwa muda wote, kila mchezaji ana timu yake.
“Madai yanayoenezwa na baadhi
ya vyombo vya habari kuhusu vitendo hivyo yametuchafua sana. Tunaomba kama kuna
mtu ana ushahidi na hilo atueleze kuliko kuendelea kutuchafua,” amesema.
Beyonce and Jay-Z Double Date with Kanye West and Kim Kardashian at BET Awards 2012
Singer Beyonce, rappers Jay-Z and Kanye West and television personality Kim Kardashian attend the 2012 BET Awards at The Shrine Auditorium on July 1, 2012 in Los Angeles, California.
Tom Cruise and Katie Holmes Divorce announcement
More of Tom Cruise and Katie Holmes separation drama unfolds as rumors recently surfaced claiming the Mission: Impossible actor, 49, has plans to file his own set of divorce papers in California as early as the upcoming week.
Though Holmes, 33, officially announced her split on Friday sought for sole custody of the couple six-year-old daughter Suri Cruise, reports say that the Jack & Jill actress may be forced to move the divorce proceedings to the west coast as she allegedly does not meet the residency requirements for the filing.JULY 2012 COVERS
Blake Lively Covers July 2012 Marie Claire Magazine
Emma Stone by Mario Testino for Vogue US July 2012
Eva Mendes UK Marie Claire July 2012 Cover
Selena Gomez Elle Magazine Covers July 2012
David Beckham Elle UK Magazine July 2012 covers
Sunday, July 1, 2012
Subscribe to:
Posts (Atom)