El Salam Wau ya Sudan Kusini na Atletico ya Burundi zinatarajiwa kuwa timu za kwanza kuwasili nchini kushiriki michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame).
Michuano hiyo inaanza kutimua vumbi Jumamosi (Julai 14 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ikishirikisha timu kumi na moja akiwemo bingwa mtetezi Yanga na makamu bingwa Simba.
Kikosi cha El Salam Wau ambacho kitawasili kesho alfajiri (Julai 11 mwaka huu) kwa ndege ya Ethiopia Airlines kikitokea Juba kupitia Addis Ababa, Ethiopia kikiwa na wachezaji 18 na viongozi saba.
Wachezaji wanaounda kikosi hicho ni Khamis Leone Uso Wani (nahodha), Adheil Bugwic Jongkor Bugwic, Edward Joram Simon Julio, Fidel Andrea Fides Fas, Ismael Musa Juma Ismael, James Anei Matheli Anei, Jervas Ayo Abdalla Ayak, Khamis Doshama Ulama Andel na Meki Sultan Berema Kuku.
Wengine ni Moga Emmanuel Androga, Mubarak Mohammed Saleh Omer, Ndili Rabeh Nasir Hozi, Nizir Rihan Taban Talib, Oliver Paul Kangi Akok, Rabie Mohammed Abubakar Hassan, Rufino Joseph Uras Ambros, Santino Makuei Uyu Upio, Thomas Rufino Thomas Diakon.
Nayo Atletico inatarajiwa kuwasili kesho (Julai 11 mwaka huu) kwa usafiri wa barabara. Timu hiyo inakuja kwa usafiri wa basi lake ambalo pia italitumia kwa muda wote itakapokuwa kwenye mashindano.
Wakati El Salam Wau itafikia kwenye hoteli ya Rungwe iliyoko maeneo ya Kariakoo, Atletico itakuwa Lunch Time Hotel iliyoko Mabibo.
Timu zinazotarajiwa kuwasili keshokutwa (Julai 12 mwaka huu) ni Mafunzo ya Zanzibar kwa boti saa 9 alasiri, Vita Club ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (RDC) itatua saa 1.20 usiku kwa Kenya Airways. Timu nyingine itakayowasili siku hiyo jioni ni URA ya Uganda.
WATANGAZAJI KWA ‘SCREEN’ KUBWA KOMBE LA KAGAME
Wakati wa michuano ya Kombe la Kagame itakayofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia Julai 14-28 mwaka huu, screen kubwa iliyoko uwanjani itatumika kwa matangazo ya biashara na ujumbe mbalimbali kwa washabiki watakaoshuhudia mechi hizo.
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linakaribisha kampuni na wadau mbalimbali wanaotaka kuweka matangazo yao wakati wa michuano hiyo itakayoshirikisha klabu kumi na moja kutoka ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati.
Muda wa kurushwa matangazo hayo yanayotakiwa kuwa kwenye mfumo wa DVD ni kabla ya mechi kuanza, wakati wa mapumziko na baada ya mechi. Matangazo hayo yanatakiwa kuwa ya sekunde 60 (dakika moja) au sekunde 30 (nusu dakika).
RAMBIRAMBI MSIBA WA MWENYEKITI FAM
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mara (FAM), Fabian Samo kilichotokea leo asubuhi (Julai 10 mwaka huu).
Samo ambaye Novemba 13 mwaka jana alichaguliwa kwa kipindi cha pili mfululizo kuwa Mwenyekiti wa FAM katika uchaguzi uliofanyika wilayani Rorya alikuwa amelazwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dar es Salaam akisumbuliwa na maradhi ya figo.
Taratibu za mazishi ya Samo ambaye alikuwa mjumbe wa Kamati ya Ukaguzi wa Hesabu (Internal Audit Committee) ya TFF ikiwemo siku atakayozikwa bado zinafanywa na familia yake.
Samo alitoa mchango mkubwa katika maendeleo ya mpira wa miguu mkoani Mara na Tanzania kwa ujumla, vitu ambavyo vilichangia kuchaguliwa kwake tena kuiongoza FAM.
Msiba huo ni pigo kwa familia ya Samo, FAM, TFF na mchezo wa mpira wa miguu kwa ujumla nchini kutokana na mchango na mawazo aliyotoa kwa kipindi chote alichokuwa kiongozi.
TFF inatoa pole kwa familia ya marehemu Samo, FAM, jamaa na marafiki na kuwataka kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki cha msiba huo mzito. Pia TFF itatoa ubani wa sh. 200,000 kwa familia ya marehemu kama rambirambi zake
.
Mungu aiweke roho ya marehemu Samo mahali pema peponi. Amina
KOZI YA MAKOCHA WA GRASSROOTS
Kozi ya makocha wa mpango wa grassroots unaolenga wachezaji mpira wa miguu (wasichana na wavulana) wenye umri kuanzia miaka 6-12 imeanza leo (Julai 10 mwaka huu) kwenye ukumbi wa Msimbazi Center, Dar es Salaam.
Wakufunzi kutoka Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) ndiyo wanaoendesha kozi hiyo iliyofunguliwa na Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Angetile Osiah.
Kozi hiyo itakayomalizika Julai 15 mwaka huu inashirikisha washiriki 35, na mwendelezo wa ile ya awali iliyofanyika Desemba 14-17 mwaka jana jijini Dar es Salaam.
Gouinden Thandoo kutoka Mauritius ni mmoja wa wakufunzi wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) wanaoendesha kozi hiyo.
Tuesday, July 10, 2012
President Kikwete arrives in London for a ground breaking International Family Planning Summit
President Jakaya Mrisho Kikwete is received at the Regency Hyatt Churchhill hotel in London today June 10, 2012 ready to attend a two-day a ground breaking International Family Planning Summit. The Summit is scheduled to launch a Global Movement to give an additional 120 million women in the World’s poorest countries, access to lifesaving family planning information, services and supplies by 2020.
The United Kingdom’s Government and the Bill & Melinda Gates Foundation, with the support of UNFPA and other partners, are hosting the summit, whose envisaged increased access will enable these women and girls to choose whether, when and how many children to have.
This Summit is a collective opportunity to generate global commitments to increase access to family planning and, in doing so, accelerate the achievement of MDGs 4 (reducing child mortality) and 5 (improving maternal health) – including MDG target 5b (reproductive health) – as well as MDG target 6a (HIV prevention).
It will build on the momentum created by the UN Secretary General's Global Strategy for Women's and Children's Health, “Every Woman, Every Child”, and the innovative public-private and civil society partnerships that are developing through the Reproductive Health Supplies Coalition (RHSC) and their Hand to Hand Campaign.
Leaders from developing and developed countries, donors, civil society groups and the private sector will come together behind a simple vision: to give women in the developing world the same access to lifesaving family planning as women in the developed world.
Monday, July 9, 2012
Kourtney Kardashian Welcomes New Baby Girl, Penelope!
There's a new Kardashian gal in the family – and her name doesn't start with a K!
Kourtney Kardashian and longtime boyfriend Scott Disick welcomed their second child to the family last night, they confirmed to E! News.The 33-year-old famous sister of Kim and Khloe confirmed her excitement about the happy arrival of her baby girl.
"Scott and I are overjoyed to welcome our precious angel Penelope Scotland Disick into our lives," Kourtney said. "We are forever blessed. Mommy and baby are resting comfortably."
MPAMBANO WA WEMA SEPETU VS JACQULINE WOLPER
Kocha wa Wema Sepetu, Rashid Matumla akimvua koti bondia wake tayari kuanza mpambano na Jacquline Wolper
Wema(kushoto) akipambana na Wolper
Ngumi si mchezo, Wema akikimbia kuogopa kuchakazwa sura na mpinzani wake
Refa John Chagu (katikati), akitangaza matokeo kuwa mabondia hao wametoka sare yaani ngumu drooo.
Michezo ni furaha, mabondia Wema Sepetu na Jacquline Wolper wakikumbatiana baada ya pambano hilo, lakini wakionesha alama ya Freemason, sisi hatujui wamo amaaaa?
Sunday, July 8, 2012
Usher’s Stepson Declared Brain Dead Following Jet Ski Accident
Following a tragic jet ski accident, Usher‘s 11-year-old stepson Kyle Glover has been declared brain dead by doctors.
On Saturday, Glover was reportedly sitting in an inner tube on Lake Lanier in Georgia when he was struck in the head by a passing jet ski driven by an unidentified 38-year-old man.According to TMZ, Glover showed no brain activity since his hospital arrival and is currently on life support.
Usher’s estranged wife, Tameka Foster, has reportedly been by the child’s beside all weekend.
While more details have yet to emerged – including if Foster and the boy’s biological father, Atlanta clothier Ryan Glover, will take Kyle off life support — the “Yeah” singer’s pals have offered their support through Twitter.
Rihanna Covers August 2012 Issue Of Harper’s Bazaar
Rihanna is the cover girl for an upcoming issue of the high end fashion bible Harper’s Bazaar. The cover image and photo spread leaked, and there appears to be two separate covers, which these women’s mags often do. One cover is reserved for subscribers, while the other lands on the newsstand.
Subscribe to:
Posts (Atom)